Pageshttps://www.insidehighered.com/views/2020/02/05/why-institutions-should-continue-support-their

Graduation

Graduation
From left: Jumanne Hussein, Dr.Suru, Mzee Gantala, Dr. Masoud during the graduation ceremony held on 26th November, 2015 at Chimwaga Hall, Dodoma

Friday, September 20, 2013

vyombo vya Habari, Ukatili wa Kijinsia na Mabadiliko!

Tamwa: Vyombo vya habari vimeleta mabadiliko nchini

CHAMA cha Waandishi wa Hhabari Wanawake Tanzania (TAMWA), kimesema vyombo vya habari vimeleta mabadiliko makubwa katika jamii kwa kufichua masuala ya ukatili wa jinsia unaoendelea nchini. Akizungumza na MTANZANIA Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Valeria Msoka alisema vyombo vya habari vimeweza kubadili jamii kwa kuleta mabadiliko chanya kwa kuandika masuala ya unyanyasaji wa wanawake na watoto na kama yangeendelea kingepatikana kizazi kisichojua haki zake.
“Tumeridhishwa na michango yenu, nyie wahariri pamoja na waandishi wa habari za wanawake na watoto.
“Tunaona matatizo mengi katika jamii ya kuteswa na kunyanyapaliwa kwa watoto wa kike na wanawake kwa ujumla yamepungua ingawa kuna baadhi ya sehemu bado ukandamizaji upo lakini tuna imani kadiri jamii inavyopatiwa taarifa itazidi kuelewa na litapungua kama siyo kuisha kabisa,” alisema Msoka.
Aliwataka watunga sera kuhakikisha sheria za kulinda haki za wanawake zinazingatiwa na zinapoonyesha kuna upungufu zirekebishwe mapema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TAWLA), Tike Mwambipile aliiomba Serikali iwe na chombo au taasisi maalumu itakayojihusisha na masuala ya ijinsia tu.
Alisema katika kipindi hiki cha kutoa maoni ya Rasimu ya Katiba Mpya, inafaa wajitokeze kwa wingi kuzungumzia masuala wanayoyaona hayafai kuwekwa katika Katiba, kwa kufanya hivyo itakuwa njia mojawapo ya kupata kile wanachokitaka.
Kuhusu utawala bora, alisema wanawake wamekuwa wakinyanyaswa kwa kuombwa rushwa ya ngono kisha wapatiwe kile wanachokihitaji, hivyo amewaomba wasivumilie bali watoe taarifa katika vyombo vya habari na kwingineko kwa ajili ya kukomesha hali hiyo.
Chanzo: Gazeti la Mtanzania

No comments:

Followers

UNGANA NA ULIMWENGU WA SELFIE

Habari Bayana

News Alerts