Mvietnamu akamatwa na pembe za kifaru nchini Kenya
Septemba 18, 2013
Maafisa wa usalama katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa ya Jomo
Kenyatta siku ya Jumanne (tarehe 17 Septemba) walimtia mbaroni mtu mmoja
kutoka Vietnam akiwa na pembe tano za kifaru zenye uzito wa kilo 20,
Capital FM ya Kenya iliripoti.
Le Manh Cuong, mwenye umri wa miaka 29, alikuwa njiani kutoka Msumbiji kwenda Hong Kong akiwa amebeba pembe za kifaru, ambazo alizitia katika katika mkoba wake wa safari uliokuwa umewekwa vipande vya godoro, alisema msemaji wa Idara ya Wanyamapori ya Kenya (KWS) Paul Muya.
Le alitiwa mbaroni kwa ushirikiano wa timu ya usalama inayoundwa na Kitengo cha Polisi cha Viwanja vya Ndege vya Kenya, maafisa wa Forodha, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Kenya, shirika la ndege la Kenya Airways na KWS. Atafikishwa katika mahakama hya Makadara siku ya Jumatano.
Muya alisema kuwa mwaka huu wageni 39, wakiwemo Wavietnam tisa na Wachina 19, wamekamatwa kwa magendo ya bidhaa harama ya wanyamapori nje ya nchi.
“Mapambano yanaendelea na hatutarudi nyuma hadi tushinde vita dhidi ya ujangili,” alisema.
Le Manh Cuong, mwenye umri wa miaka 29, alikuwa njiani kutoka Msumbiji kwenda Hong Kong akiwa amebeba pembe za kifaru, ambazo alizitia katika katika mkoba wake wa safari uliokuwa umewekwa vipande vya godoro, alisema msemaji wa Idara ya Wanyamapori ya Kenya (KWS) Paul Muya.
Le alitiwa mbaroni kwa ushirikiano wa timu ya usalama inayoundwa na Kitengo cha Polisi cha Viwanja vya Ndege vya Kenya, maafisa wa Forodha, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Kenya, shirika la ndege la Kenya Airways na KWS. Atafikishwa katika mahakama hya Makadara siku ya Jumatano.
Muya alisema kuwa mwaka huu wageni 39, wakiwemo Wavietnam tisa na Wachina 19, wamekamatwa kwa magendo ya bidhaa harama ya wanyamapori nje ya nchi.
“Mapambano yanaendelea na hatutarudi nyuma hadi tushinde vita dhidi ya ujangili,” alisema.
No comments:
Post a Comment